Kiungo wa zamani wa klabu ya soka ya Arsenal Paul
Merson ameitaka klabu ya Arsenal kumsajili kiungo wa Southampton Victor Wanyama
katika kipindi cha dirisha dogo la usajili mwezi Januari mwakani.
Klabu ya Tottenham ilishindwa kumnasa kiungo huyo
mwenye uraia wa Kenya na inaelezwa kuwa sasa wanajipanga kutenga mezani dau linguine.
Merson amesema Wanyama ni mchezaji sahihi mwenye
nguvu na mwenye uwezo wa kutawala eneo la katikati kwa kuwapasia Ozil, Sanchez,
Cazorla.
0 comments:
Post a Comment