Ahmed Ally akiwa 'kapozi' na mkewe |
Na Arone Mpanduka
Hayawi hayawi na sasa yamekuwa. Hivyo ndivyo
ilivyotokea kwa mwandishi wa habari za michezo Ahmed Ally ambaye ameachana na
ukapera na kufunga ndoa jana(Ijumaa).
Ahmed Ally ambaye ni mwandishi wa habari za michezo
kutoka katika kituo cha Televisheni cha Star TV na Radio Free Afrika, pia ni
mwanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo nchini (TASWA)
Kitendo cha Ahmed kufunga ndoa hiyo ya Kiislamu kimeongeza
idadi ya waandishi wa bahari za michezo waliojitosa na kufunga ndoa kwa mwaka
huu.
Miongoni mwa waandishi hao ni Michael Matemanga,
Khatim Naheka, Michael Momburi (wote kutoka Kampuni ya Mwananchi Communications
Limited) pamoja na Arone Mpanduka (Radio Tumaini) ambaye pia ni mmiliki wa
MPANDUKA BLOG.
Disemba 26 mwaka huu, mwandishi mwingine wa habari za michezo Wilbert Molandi anatarajia kufunga ndoa.
Molandi kwa sasa anafanya kazi katika gazeti la michezo la Champion.
Habari za uhakika ambazo MPANDUKA BLOG imezipata
zinaeleza kwamba kabla ya mwaka huu kumalizika waandishi wengine wa habari za
michezo wataoa na kuolewa.
Mke wa Ahmed Ally katika 'pozi' tofauti tofauti |
0 comments:
Post a Comment