KILI STARS IPO TAYARI KWA CHALLENGE CUP



Timu ya soka ya taifa ya Tanzania Bara kesho itashuka dimbani huko nchini Ethiopia kukipiga dhidi ya Somalia katika mchezo wa Kundi A wa michuano ya Chalenji inayohusisha timu kutoka nchi za Afrika Mashariki na Kati maarufu kama CECAFA Challenge Cup.

Mchezo huo utapigwa kuanzia saa nane mchana.

Tayari kikosi cha Taifa Stars kipo nchini Ethiopia kikisubiri mashindano hayo chini ya kocha mkuu Abdallah ‘King’ Kibadeni ‘Mputa’

Asilimia kubwa ya wachezaji wanaounda kikosi hicho wanatoka Taifa Stars, kikosi ambacho kilicheza na Algeria, lengo likiwa kumpunguzia kocha kazi kwa sababu wachezaji wengi wameiva kimazoezi.
Kibadeni


Nayo Kenya watakipiga na mabingwa wa kihistoria, Uganda kesho hiyo hiyo majira ya jioni. 

Mechi za mzunguko wa kwanza wa makundi zitakamilishwa keshokutwa ambapo Sudan Kusini watamenyana na Djbouti kabla ya Sudan na Malawi kufuatia baadaye.

Baada ya mechi za makundi kufikia tamati, Robo Fainali zitafuatia Novemba 30 zikihusisha timu mbili za juu kutoka kila kundi na washindi watatu bora wawili kwa makundi yote. 

Nusu Fainali zitafanyika Desemba 2 na 3, wakati mechi za kusaka Mshindi wa tatu na Fainali zitafanyika Desemba 5, mwaka huu na huo utakuwa mwisho wa mashindano.

RATIBA
Novemba 21, 2015
Burundi Vs Zanzibar Saa 8:00 mchana
Ethiopia Vs Rwanda Saa 11:00 jioni

Novemba 22, 2015
Somalia Vs Tanzania Saa 8:00 mchana
Kenya Vs Uganda Saa 11:00 jioni

Novemba 23, 2015
Sudan v Djbouti Saa 8:00 mchana
Sudan v Malawi Saa 11:00 jioni

MAKUNDI:
Kundi A; Ethiopia, Rwanda, Tanzania Bara na Somalia.
Kundi B; Kenya, Uganda, Burundi na Zanzibar.
Kundi C; Sudan, Sudan Kusini, Malawi na Djibouti.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment