Ethiopia |
Bao la kujifunga la beki wa Kilimanjaro Stars Salum
Mbonde leo limewasaidia Ethiopia kutinga hatua ya robo fainali baada ya kupata
sare ya 1-1 katika mchezo wa mwisho wa kukamilisha hatua ya makundi wa michuano
ya Chalenji inayoendelea huko nchini Ethiopia.
Kilimanjaro Stars leo iliingia uwanjani huku ikiwa
haina cha kupoteza baada ya kuwa tayari na pointi 6 kibindoni na kufuzu kutinga
hatua ya robo fainali isipokuwa ilitaka kushinda ili kulinda heshima.
Kili Stars ilikuwa ya kwanza kupata bao lililofungwa
na Simon Msuva ambapo bao hilo la pili kwake katika mashindano ya mwaka huu kwa
kichwa dakika ya 51 akimalizia krosi maridadi ya beki wa kushoto, Mohammed
Hussein ‘Tshabalala’.
Baada ya bao hilo mnamo dakika ya 90 ndipo Mbonde alipojifunga
katika harakati za kuokoa mpira uliopigwa na Mohamed Naser.
Kwa mujibu wa hesabu za kundi hilo la A, Ethiopia
ilihitaji sare tu dhidi ya Kili Stars ili isonge mbele na si kinyume na hapo,
jambo ambalo limetokea.
Baada ya mechi hiyo, hatua ya robo fainali itaanza
rasmi keshokutwa ambapo..
Tanzania Bara Vs Ethiopia
0 comments:
Post a Comment