AZAM FC YABANWA TENA TANGA



Timu ya soka ya Azam FC jioni ya leo imetoka sare ya bao 1-1 na wenyeji African Sports ya jijini Tanga katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani.

Hiyo ni mechi ya pili kwa Azam ambayo inajiandaa na Ligi Kuu Tanzania Bara.

Hapo juzi Azam ilitoka sare ya 1-1 na Mgambo JKT katika mechi yake ya kwanza ya ziara hiyo ya kimazoezi jijini Tanga.

Mechi ya leo ndiyo imehitimisha ziara hiyo ya Tanga ambapo kesho Jumapili Azam itarejea nyumbani Chamazi Dar es salaam.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment