JIKUMBUSHE MATUKIO YA MICHEZO KWA MWAKA 2015



JANUARI
Simba yatwaa ubingwa wa Kombe la Mapinduzi baada ya kuifunga Mtibwa Sugar penati 4-3 baada ya suluhu ya 0-0 katika dakika 120.
Shujaa wa mchezo alikuwa kipa wa Simba kwa wakati huo Ivo Mapunda baada ya kupangua moja ya penati hizo.(Hiyo ilikuwa ni usiku wa Januari 13, siku ya Jumanne kwenye dimba la Aman)

FEBRUARI
Februari 2 bondia Francis Cheka alihukumiwa kwenda jela kutumikia kifungo cha miaka mitatu.


Hukumu hiyo ilitolewa Morogoro baada ya bodnia huyo kubainika kwa kosa la kumpiga mfanyakazi wa Bar huko Morogoro, tukio ambalo lilitokea mwaka 2014.

February 6 mchezaji wa Mbeya City Juma Nyosso alifungiwa mechi 8 kwa kosa la kumdhalilisha aliyekuwa mchezaji wa Simba Elias Maguli.
Nyosso alifanya hivyo kwenye mchezo kati ya Mbeya City na Simba.

MACHI
Machi 25 mwaka huu mwanachama wa ‘Simba Ukawa’ Hassan Msumari nusura apate kichapo baada ya kwenda katika jengo la Yanga kwa lengo la kuzungumza na waandishi wa nabari waliokwenda huko kwa lengo la kufanya mkunano na uongozi wa Yanga.

Msumari ambaye mwenyekiti wa Chama cha Muziki wa Dansi nchini alikwenda Yanga kwa lengo la kukutana na waandishi ili awape habari zinazohusu chama hicho lakini katika hali ya kushangaza Yanga walidai kwamba Msumari alitumwa na klabu ya Simba ili kwenda kufanya ushirikina klabuni hapo.

Hata hivyo gari la polisi ilikuja na kumuokoa ili aipewe kichapo na wanachama wa Yanga waliokuwepo klabuni hapo wakiongozwa na mzee Akilimali.

Machi 27 bondia Mohamed Matumla alishinda pambano la masumbwi la raundi 10 kwa kumchakaza Mchina Wang Xiu Hua.Pambano lilifanyika ukumbi wa Diamond Jubilee.

APRILI
Aprili 27 Yanga ilijitangazia ubingwa wa Ligi Kuu mapema baada ya kuinyuka Polisi Moro mabao 4-1 kwenye mechi iliyopigwa uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Yanga ilitawazwa bingwa baada ya mechi hiyo licha ya kuwa ilibakisha mechi kadhaa za kumaliza Ligi.

MEI
Mei 8 mwaka huu TFF ilimpiga faini ya shilingi milioni 5 msemaji wa Yanga Jerry Murro kwa kosa la kumrushia maneno yasiyofaa aliyekuwa kaimu mtendaji mkuu wa Bodi ya Ligi.


Kisa kilikuwa ni kupinga kanuni ya ajabu ya mchezaji mwenye kadi mbli za njano kuruhusiwa kuchagua mchezo wa kutumikia adhabu.

Mwishoni mwa mwezi Mei mwaka huu, aliyekuwa kiungo wa Simba Ramadhan Singano aliibua mjadala mzito kwenye vyombo vya habari baada ya kulalamika kwamba Uongozi wa Simba ulighushi mkataba wake.

Singano alidai kwamba mkataba wake ni wa miaka miwli na ulikuwa uishe mwaka huu lakini Simba ilidai Messi kasaini mkataba wa miaka mitatu hivyo hakuna haja ya kumuongezea mkataba mpya ilhali alikuwa na mwaka mmoja mbele.

JUNI
Katika hali ya kushangaza Juni 9 mwaka huu, TFF ilitoa maamuzi ya kutatanisha juu ya sakata la Singano na Simba. Katibu mkuu wa TFF Celestine Mwesigwa alisema wamezitaka pande zote mbili kukaa na kukubaliana kumsainisha mkataba mpya mchezaji huyo

Hata hivyo Singano alionekana kutoridhishwa na maamuzi hayo na kusema kwamba anamuachia Mungu

Juni 23 Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania – TFF, Jamal Malinzi alizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa hoteli ya Tansoma eneo la Gerezani na kumtangaza Charles Mkwasa kuwa kocha mkuu wa muda baada ya Mart Nooij kutimuliwa.

Mkwasa alipewa mkataba wa muda wa miezi 3 hadi Septemba 30 na kisha kupewa wa kudumu.


JULAI
Julai 9 mwaka huu Rais mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete alisema watu wanamfikiria vibaya kwamba akienda kutazama mechi za Timu ya Taifa Stars huwa hazifanyi vizuri.

Maneno hayo aliyasema wakati akivunja rasmi Bunge la 10 mjini Dodoma ili kupisha mchakato wa uchaguzi mkuu wa Rais Wabunge na Madiwani
Julai 23 mwaka huu Yanga ilianza rasmi hadithi za uchaguzi baada ya muda wa viongozi wa kuchaguliwa kumalizika rasmi.

AGOSTI
Agosti 2 Azam FC ilitwaa kombe la Kagame kwa mara ya kwanza kabisa tangu ianzishwe mwaka 2007 baada ya kuinyuka Gor Mahia mabao 2-0 katika mchezo wa fainali.

Agosti 17 mwaka huu Baraza la Sanaa la Taifa BASATA lilitangaza rasmi kulitoa kifungoni shindano la Miss Tanzania.

Shindano hilo lilipigwa stop Disemba 22 mwaka jana kufuatia skendo la kughushi umri ililomkumba Sitti Mtemvu mwishoni mwa mwaka jana na kulazimika kuvua taji na kumkabidhi Lilian Kamazima

SEPTEMBA
Jumamosi ya Sept 26 Mchezaji chipukizi wa timu ya vijana ya Coastal Union ya Tanga, Mshauri Salim alifariki dunia baada ya kuanguka kwenye Uwanja wa Mkwakwani kufuatia kugongana na mchezaji mwenzake.

Tukio hilo lilitokea katika mchezo wa timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Coastal Union dhidi ya Eagles Academy uliotangulia kabla ya mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya Coastal na Mwadui FC ya Shinyanga uliomalizika kwa sare ya 0-0.

Septemba 30 mwaka huu mchezaji wa Mbeya City Juma Nyosso alipata adhabu nyingine tena kwa kosa lilelile la udhalilishaji ambapo safari hii alimdhalilisha mchezaji wa Azam FC John Bocco.

Nyosso alifungiwa kutojihusisha na soka kwa kipindi cha miaka miwili baada ya kumdhalilisha Bocco kwenye mchezo wa Ligi kuu kati ya Mbeya City na Azam uliopigwa Jumapili ya Sept 27.


OKTOBA
Oktoba 2  Bondia Cosmas Cheka, alifanikiwa kuingia kwenye rekodi ya mabondia wa Tanzania waliobeba ubingwa wa dunia.

Cheka ambaye ni mdogo wa bingwa mwingine wa dunia, Francis Cheka alimtwanga bondia wa Thailand huko nchini Thailand na kubeba ubingwa huo wa dunia.


Licha ya kwenye rekodi ya mabondia waliowahi kubeba ubingwa wa dunia akiwemo kaka yake Cheka, pia ameingia kwenye rekodi ya mmoja wa mabondia waliobeba ubingwa wa dunia wakiwa nje ya ardhi ya Tanzania.

Wengine waliowahi kubeba ubingwa wa dunia wakiwa nje ya ardhi ya Tanzania ni marehemu Magoma Shabani aliyebeba ubingwa wa dunia wa WBU nchini Italia.

NOV
Novemba 17 mwaka huu(Jumanne) aibu ya mwaka iliikumba Taifa Stars kwa kunyukwa mabao 7-0 na Algeria katika mchezo wa kuania kupangwa kwenye makundi ya kufuzu kwa fainali za kombe la dunia za mwaka 2018.

Mchezo huo ambao ulipigwa nchini Algeria uliifanya Stars iondoshwe kwenye kinyang’anyiro hicho baada ya mchezo wa awali timu zote kutoka sare ya 2-2.

Novemba 19 mwaka huu kocha Kassim Majaliwa ambaye pia ni Mbunge wa Ruangwa alitangazwa rasmi kuwa Waziri mkuu mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Majaliwa alipata nafasi hiyo baada ya kuthibitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa wingi wa kura za ndiyo baada ya jina lake kuwasilishwa Dodoma na Rais John Pombe Magufuli.

Majaliwa ni mmoja kati ya watu wanaopenda michezo, jambo ambalo lilimfanya asomee ukocha na kupata Leseni B ya Shirikisho la soka Barani Afrika CAF.

Kufuatia kuwa na taaluma hiyo, Majaliwa ana uwezo wa kufundisha timu yoyote ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

DEC
Disemba 13 Timu ya taifa ya kuogelea ilitwaa medali 45 kwenye michuano ya Afrika iliyofanyika Disemba 13 hadi 16 nchini Uganda.

Timu hiyo ilishinda medali 12 za dhahabu, 22 za fdha na n11 za shaba.
Disemba 28 Yanga ilifanya maamuzi magumu kwa kumtimua Haruna Niyonzima baada ya kuona kwamba mchezaji huyo amekiuka masharti ya mkataba.

KIMATAIFA
Mchezaji wa Bayern Munich Robert Lewandowski alifunga mabao matano ndani ya dakika 9 dhidi ya Wolfsburg(Sept 22)

Sepp Blatter na Michel Platini walipigwa mvua ya kifungo cha miaka 8 na kamati ya maadili ya FIFA bada ya kubainika kuwa walifanya ubadhilifu.


Watanzania Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu walibeba kombe la klabu bingwa Afrika.


Timu ya soka ya taifa ya wanawake ya USA ilichukua kombe la dunia kwa mara ya tatu na kuwa timu iliyochukua kombe hilo mara nyingi.

Barcelona imecukua jumla ya makombe matano kwa mwaka huu.

Leicester City kukaa kileleni mwa EPL sikukuu ya Krismasi

Cristiano Ronaldo alivunja rekodi ya ufungaji wa muda wote ndani ya Real Madrid ambayo ilikuwa ikishikiliwa na Raul Gonzalez mwenye magoli 323.

Chelsea yatwaa taji la Ligi kuu England.Iliifunga Crystal Palace bao 1-0.


Pambano la masumbwi la bondia Floyd Mayweather na Manny Paquiao ambapo Mayweather alishinda.

Chelsea yamtimua Jose Mourinho

Uholanzi yashindwa kuuzu michuano ya Euro 2016.

MATUKIO HAYA YAMETAYARISHWA NA ARONE MPANDUKA
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment