PISTORIUS HATARINI KUOZEA JELA

Mahakama ya Juu nchini Afrika Kusini imempata mwanariadha mlemavu Oscar Pistorius na hatia ya mauaji.

Mahakama hiyo imekubali rufaa iliwasilishwa na upande wa mashtaka ikitaka Pistorius apatikane na hatia ya mauaji, ambayo adhabu yake ni kali zaidi kuliko ya kuua bila kukusudia.

Jaji Lorimer Leach amesema mwanariadha huyo anafaa kurejeshwa kwa jaji aliyemhukumu ili apokee adhabu ya kosa la mauaji.

Pistorius alimuua mpenzi wake Reeva Steenkamp Februari 2013 baada ya kufyatua risasi kupitia mlango wa choo.

Pistorius akiwa na Reeva ambaye alikuwa mwanamitindo
Amekuwa akitumikia kifungo cha nyumbani baada ya kukaa mwaka mmoja gerezani kwa kosa la kuua bila kukusudia.

Awali, ilikuwa imeripotiwa kimakosa kwamba rufaa hiyo ilikuwa imetupwa na angeendelea kutumia kifungo cha kuua bila kukusudia.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment