ANDY MURRAY AANZA VEMA MADRID OPEN




Mwingereza Andy Murray ameanza vyema kutetea taji lake katika michuano ya Madrid Open kwa ushindi wa seti 7-6 7-3 3-6 na 6-1 dhidi ya Radek Stepanek.

Ilichukua muda wa saa mbili na dakika 16 kwa Murry kumshinda Stepanek raia wa Czech mwenye miaka 37.

Mapema kwenye mchezo wa awali Muhispaniola Rafael Nadal alimshinda Andrey Kuznetsov wa Urusi kwa seti 6-3,6-3.

Nadal ambaye alifungwa alipocheza na Murray katika fainali za mwaka jana anaweza kukutana tena na mpinzani wake huyo katika nusu fainali za mwaka huu.

Kinara nambari moja wa mchezo huo duniani Novak Djokovic atashuka dimbani siku ya jumatano kukipiga dhidi ya Borna Coric kutoka Crotia.

Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment