MAKOCHA WAWILI WATUA NCHINI KUINOA AZAM FC

Makocha wawili kutoka klabu ya Deportivo Tenerife ya Hispania wamewasili jioni ya leo kwa ajili ya kuja kufanya mazungumzo ya kusaini Mkataba wa kufundisha Azam FC.
Makocha hao Jonas Garcia Luis na Zebensul Hernandez Rodriguez wamewasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam Saa 10:00 jioni kwa ndege ya Emirates na kupokewa na Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba.

Mara baada ya kuwasili JNIA, makocha hao walisema kwamba wanatarajia kupata mwongozo wote kutoka wenyeji wao na wasingeweza kuzungumza mambo mengi.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment