TFF YAIPOKA AZAM POINTI 3 LEO, KISA....





Siku moja baada ya kutoka sare ya 2-2 na JKT Ruvu, Azam FC imekumbana na balaa lingine hii leo baada ya kupokwa pointi tatu na mabao matatu kwa kosa la kumtumia beki wao, Erasto Nyoni aliyekuwa na kadi tatu za njano.  

Taarifa za uhakika zilizoifikia MPANDUKA BLOG zinasema katika mechi namba 156 iliyozikutanisha Mbeya City dhidi ya Azam kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya, Azam ilimchezesha Nyoni kinyume na sheria huku wakitambua kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Adhabu hiyo inafuatia ushindi wa Azam wa mabao 3-0 iliyoupata Februsri 20 mwaka huu kwenye dimba la Sokoine Mbeya huku ndani yake akichezeshwa Erasto Nyoni aliyekuwa na kadi tatu za njano.

Licha ya kushinda Azam wamepoteza mchezo ule na sasa Mbeya City imepewa pointi tatu na mabao matatu huku benchi la ufundi la Azam likionywa kuwa makini ili jambo hilo lisiwatokee tena.

Hali hiyo inazidi kuiachia Yanga nafasi ya kutwaa taji la Ligi Kuu msimu huu.

Taarifa zaidi zitafuata…

NB; Pia tegea sikio kipindi cha michezo cha kutoka viwanjani cha Redio Tumaini kuanzia saa 1;00 hadi 1;30 usiku wa leo kupitia 96.5 FM ama nje ya Dar www.tumainimedia.com
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment