BAADA YA KAMBI YA ULAYA KUOTA MBAWA, CHEKA AFANYA UAMUZI HUU



Na Arone Mpanduka

Kufuatia kambi yake ya Ulaya kuota mbawa,bondia wa ngumi za kulipwa nchini Francis Cheka amesema atafanya mazoezi yake hapa hapa nchini ili kuhakikisha anamtwanga mpinzani wake Thomas Mashali siku ya Disemba 25 mwaka huu.

Cheka atavaana na Mashali katika pambano lisilo la ubingwa litakalofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro huku lengo likiwa ni kukata ngebe kwa pande zote mbili.

Akizungumza na mpanduka.blogspot.com kwa njia ya simu kutoka Morogoro, Cheka alisema kuyeyuka kwa kambi ya Uingereza hakutoweza kumfanya asijiandae dhidi ya pambano hilo.

“Nilipaswa kuwa Uingereza sasa hivi kujiandaa na pambano dhidi ya Mashali lakini yote heri, nipo Morogoro na nitaendelea kujiandaa nikiwa hapa na ninauhakika siku hiyo naua mtu,”alisema.

Alisema mipango ya safari yake ilikuwa inakwenda vizuri lakini dakika za mwisho alishindwa kuelewa kilichotokea na kufanya safari isiwepo tena.

Cheka alisema anashukuru kwamba kocha wake anampa mazoezi ya kutosha na mbinu mbadala za kupata ushindi.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment