KOBE BRYANT NA LAKERS HALI MBAYA, CAVALIERS, OKLAHOMA ZAPETA

Kobe Bryant




















Jahazi la Kobe Bryant na timu yake ya Lakers limeonekana kuzidi kuzama baada ya usiku wa jana kufungwa na New York Knicks kwa pointi 99-95 kwenye mchezo wa Ligi ya Mpira wa Kikapu nchini Marekani NBA.

Uwanja mzima ulionekana kumshangilia kwa nguvu pale Madison Square Garden ingawa Lakers walifungwa.

Ikumbukwe kuwa huo ndio uwanja ambao Kobe alifunga pointi zake za mwanzo za NBA takribani miaka 20 iliyopita. 

Katika kipindi hicho Bryant alifunga pointi 18.

“Naweza kukumbuka mchezo wangu wa kwanza hapa , bila kujua nini cha kutarajia na ni kipi au ni nini cha kufanya, lakini tu kuwa katika moja ya viwanja vikubwa na vinavyoheshimika ,”alisema Bryant

James alicheza na mguu mbovu kiais lakini kila alichofanya hakikutofautiana sana na yule Lebron anayecheza akiwa mzima na mwenye afya kamili.

Katika mchezo mwingine nyota LeBron James alifunga pointi  29 na kuonyesha kiwango cha juu na  kuiongoza Cleveland  Cavaliers kuichapa Pacers Indiana pointi 101-97 na kufikisha ushindi wao wa sita mfululizo.



James alipambana licha ya mguu wake kuwa na maumivu lakini kiwango chake kilikuwa imara sawa na kipindi chote anachokuwa na afya njema.

 “Nilianza mchezo vema bila maumivu yoyote na vizuri lakini nikagongwa  tena katika robo ya tatu hivyo ilikuwa inauma kwelikweli,” James alisema.

Mchezo mwingine ulishuhudia mchezaji Kevin Durant akizoa pointi 32 na ribaundi 11 wakati timu yake ya Oklahoma City ikiwapiga Phoenix Suns 124-103 na kukwepa rekodi ya kupoteza michezo mitau mfululizo. 

Russell Westbrook alikuwa na pointi 21, pasi 13 na ribaundi sita , na Enes Kanter alikuwa na pointi 21. 

Eric Bledsoe alikuwa na pointi 28 na pasi 11 kwa upande wa Phoenix Suns.
Markieff Morris alifunga pointi 19 na T.J. Warren aliongeza 17 kwa Phoenix, ambayo ilipoteza kwa mara ya tatu katika mechi nne.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment