NIGERIA MABINGWA KOMBE LA DUNIA
























Timu ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Nigeria, Golden Eaglets imetwaa ubingwa wa Dunia wa vijana wa umri wa huo baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Mali jana nchini Chile.

Ushindi huo unamaanisha kwamba Nigeria imetetea taji lao ililolitwaa miaka miwili iliyopita Falme za Kiarabu (UAE).

Mabao ya haraka haraka ya kipindi cha pili ya Victor Osimhen na Funsho Bamgboye yalitosha kukihakikishia taji hilo kikosi cha Emmanuel Amuneke, hilo likiwa taji la tano la dunia kwa U17.

Hii ni mara ya kwanza Nigeria wanatwaa taji hilo nje ya Asia, baada ya mataji yao ya awali kubeba China mwaka 1985, Japan mwaka 1993, Jamhuri ya Korea mwaka 2007 na UAE mwaka 2013.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment