MREMBO EVA CARNEIRO AOLEWA




































Ikiwa imepita miezi mitatu tangu aondoke Chelsea, daktari wa wachezaji Eva Carneiro amefunga ndoa na mpenzi wake Jason De Carteret ambaye ni mshauri na mtafiti wa mambo ya biashara.

Ndoa hiyo ambayo ilifungwa kwenye kanisa la St Patrick  mjini London, haikuhudhuriwa na mchezaji, kocha wala kiongozi yoyote wa Chelsea.

Mchezaji aliyekuwepo kwenye harusi hiyo ni golikipa wa zamani wa Chelsea Mark Schwarzer ambaye kwa sasa anaichezea klabu ya Leicester City.

Miezi michache iliyopita mrembo huyo alikwaruzana na kocha Jose Mourinho na kutimuliwa katika klabu hiyo.

Mourinho alikorofishana na Eva kwa madai kwamba alipoteza muda wakati anamtibu Eden Hazard huku Chelsea ikiwa tayari imefungwa.
Eva akikwaruzana na bosi wake Mourinho wakati alipokuwa Chelsea


Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment