TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO



Mshambuliaji wa kimataifa wa Wales Gareth Bale yu katika hatihati ya kuipa kisogo Real Madrid kufuatia kichapo cha mabao 4-0 ilichopata timu yake kutoka kwa Barcelona.Inaelezwa kuwa Manchester United inajiandaa kutenga dau kwa ajili ya kumnasa mshambuliaji huyo.(The Sun)

Inaelezwa kuwa mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo, 30, amekasirishwa na kichapo cha Jumamosi cha mabao 4-0 hivyo anataka kocha wake Rafael Benitez aondolewe na nafasi yake ichukuliwe na mtu mwingine (Daily Telegraph limeandika)

Bosi wa Liverpool Jurgen Klopp anataka kumsajili kiungo wa Lazio Lucas Biglia mwenye umri wa miaka 29 lakini atakumbana na ushindani kutoka Manchester United. (Fichajes - Hispania) 

Klabu ya Southampton inataka kumshikilia mshambuliaji wake Sadio Mane mwenye umri wa miaka 23 ili asiondoke na inataka kumuongezea mkataba mpya ili kuzima mbio za Manchester United na Chelsea juu ya mchezaji huyo. (Daily Express) 

Klabu za Manchester United na Arsenal zinamuwania beki wa Juventus Danile Rugani mwenye umri wa miaka 21.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment