YANGA SASA HAINA MPANGO WA KUSAJILI



Na Arone Mpanduka

Klabu ya soka ya Yanga imesema haina mpango wowote wa kuongeza mchezaji katika kipindi cha sasa cha dirisha dogo la usajili.

Akizungumza na mpanduka.blogspot.com jioni ya leo, Katibu mkuu wa klabu hiyo Dokta Jonas Tiboroha alisema kikosi chao kimekamilika hivyo hawaoni haja ya kuongeza wachezaji wengine.

Alisema programu ya kocha Hans van Der Pluijm haimpi nafasi ya kuongeza wachezaji wengine labda itokee dharura ya namna yoyote itakayomlazimu kubadili maamuzi yake.

“Kwa kikosi tulichonacho sidhani kama kuna ulazima wa kuongeza mchezaji yeyote.Halafu kipindi hiki ni kigumu sana kupata mchezaji kwa sababu kila mchezaji unakuta ana mkataba mrefu sana,” alisema Tiboroha

Kipindi cha dirisha dogo la usajili ambacho kilianza Novemba 15 mwaka huu kitafikia tamati Desemba 15 mwaka huu.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment