FERGUSON 'AMCHANA' ABRAMOVICH

Ferguson


Kocha wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson amesema endapo mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich atamtimua Jose Moutinho, atakuwa amefanya maamuzi ya kipuuzi na kuonyesha mfano wa uongozi mbovu.

Ferguson ambaye enzi zake aliipatia mataji mengi Man United, amemuelezea Mourinho kuwa ni miongoni mwa makocha bora wa wakati wote na kumtaka atatue matatizo yanayoikumba kampeni ya Chelsea ya kutetea taji la Ligi Kuu.

Amesema tayari tajiri huo ametimua makocha wengi katika miaka 10 iliyopita, jambo ambalo anaamini Abramovich atakuwa amejifunza kwa sasa.

Amesema Mourinho ameshinda taji la Ulaya mara mbili na pia ametwaa mataji ya Ligi za nchi kwenye kila nchi aliyokwenda.
 
Roman Abramovich
Mourinho
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment