MAN CITY AFA 2-0 JIONI HII

Benchi la ufundi la Man City likiwa limechanganyikiwa


Timu ya soka ya Manchester City jioni hii imekiona cha mtema kuni baada ya kutandikwa mabao 2-0 katika mchezo wa Ligi Kuu soka nchini England.

Mabao yote mawili ya Stoke yamefungwa na Arnautovic 7’ na 15’

Kufuatia kupoteza mchezo huo, Man City bado ipo kileleni kwa muda ikiwa na pointi 29 sawa na Leicester City ambayo ipo dimbani kuvaana na Swansea.

Endapo Leicester itashinda leo hii, itapanda tena kileleni mwa msimamo wa Ligi kwani itakuwa imefikisha pointi 32
Arnautovic akishangilia mabao yake leo

Mchoro ukionyesha jinsi Arnautovic alivyoifunga Man City bao la kwanza.Namba unazoziona ni za jenzi za wachezaji wa Stoke City
 
Jinsi Arnautovic alivyofunga bao la pili    











Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment