MPIRA WA VINYOYA KURUDI UPYA?

Katibu Desouza


Kamati ya muda ya Chama cha Mchezo wa Vinyoya Tanzania (TBA) imeiomba Kamati ya Olimpiki nchini (TOC) kuurudisha upya mchezo huo baada ya kupotea kwa miongo miwili.

Kamati hiyo iliundwa kwa amri ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT) ikiwa ni sehemu ya kupitia vyama mbalimbali vya michezo nchini na kuona utendaji wake.

BMT ilibaini udhaifu mkubwa ikiwamo kutofanyika mikutano ya kitaifa na kukosekana kwa wanachama kunakochangiwa na katiba mbovu ya chama hicho.

Novemba mwaka huu BMT iliitangaza kamati hiyo itakayodumu kwa siku 90 ikitakiwa kuhamasisha wanachama wapya ili kufanyika mkutano mkuu na kuandaa mashindano.

Akizungumza wakati wa kutangaza mashindano ya mchezo huu yanayotarajia kufanyika jijini Dar es Salaam Desemba 5-6 mwaka huu, Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Timothy Kahoho alisema, “Mchezo wa vinyoya uliing’arisha Tanzania enzi za utawala wa Mwalimu Nyerere, lakini kutokana na kukosa kuungwa mkono ulijikuta ukipotea katika medani ya kimataifa miaka 20 sasa haujashiriki katika michuano ya olimpiki”.

Kahoho alisisitiza kwamba mchezo wa vinyonya ukirudishwa na TOC utaiwakilisha Tanzania kama awali kwani kwa miaka ambayo haujashiriki umezifanya Uganda na Kenya kupanda viwango kutokana na serikali zao kuunga mkono juhudi zinazofanywa.

Mbali na hilo Kahoho alitangaza kuenzi mchango wa mwasisi wa mchezo huo nchini Marehemu Rwehabura Kente aliyefariki Machi 2015 kuanzia mwaka  ujao kutakuwa na mashindano yatakayojulikana kwa jina la Kente Cup.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa TBA, Toney Desouza alisema mashindano hayo yatawaleta pamoja wachezaji akali ya 30 kutoka Tanzania, Kenya, Uganda na Zambia kwa wanaume na wanawake (singles & doubles).

“Viwanja vitakavyotumika katika michuano hiyo mwaka huu ni Shuskunj, Badminton Institute na Khalsa SC maeneo ya Kisutu jijini Dar es Salaam,” alisema Desouza
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment