MWANARIADHA OSCAR APEWA DHAMANA, LAKINI...




Mwanariadha mlemavu kutoka Afrika Kusini Oscar Pistorius amepewa dhamana akisubiri hukumu ya mauaji ya mpenzi wake Reeva Steckhamp.
Hukumu inatarajiwa kusomwa Aprili 18 mwaka ujao.

Jaji Aubrey Ledwaba amesema hakuna hatari kwamba Pistorius anaweza kutoroka akipewa dhamana kwani alijisalimisha mahakamani mwenyewe hii leo.

Pistorius, mwenye umri wa miaka 28, ametakiwa kulipa randi 10,000 ($700) kama dhamana.

Ataendelea kutumikia kifungo cha nyumbani na atakuwa na kifaa cha kumfuatilia kielektroniki. 

Anaruhusiwa kuondoka nyumbani kati ya saa moja asubuhi hadi saa sita mchana katika eneo la nusu kipenyo la kilomita 20 kutoka kwenye nyumba anayoishi.

Pistorius pia ametakiwa kusalimisha pasipoti yake ya kusafiria kwa mahakama.

Oscar anakabiliwa na kifungo cha zaidi ya miaka 15, ingawa jaji huenda akampunguzia hukumu.

Bingwa huyo wa Olimpiki alirejea kortini leo baada ya mahakama ya rufaa kubatilisha uamuzi wa mahakama ya chini wa kumpata na hatia ya kuua bila kukusudia na badala yake ikaagiza ahukumiwe kwa mauaji.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment