TP MAZEMBE KUANZA NA AUCKLAND CITY

Mabingwa wa Afrika, TP Mazembe sasa wamejua mpinzani wao wa kwanza katika michuano ya Kombe la Dunia kwa klabu.

Mazembe inakutana na Sanfrecce Hiroshima ya Japan ambayo leo imeanza michuano hiyo vizuri kwa kuichapa Auckland City ya New Zealand.

Mabao mawili ya Minagawa na Shotani, yalitosha kuwapa ushindi wenyeji hao na sasa wanakutana na TP Mazembe Jumapili.

Watanzania Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanatarajia kuongoza mashabulizi ya Mazembe ambayo tayari ipo mjini Osaka kwa ajili ya mechi ya Jumapili.
TP Mazembe imepewa nafasi ya kuanzia robo fainali, ikishinda mechi ya Jumapili, itacheza nusu fainali desemba 16 dhidi ya River Plate ya Argentina, ikishinda, basi ndiyo fainali.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment