YANGA YAWAJUA WAPINZANI WAO KLABU BINGWA AFRIKA

Yanga


Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limeipanga Yanga kuanza na Cercle de Joachim ya Mauritius katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Yanga ndiyo mabingwa wa Tanzania na wawakilishi katika Ligi ya Mabingwa ambayo ni michuano mikubwa zaidi kwa ngazi ya klabu.

Kwa mujibu wa ratiba ya Caf, iwapo Yanga itaifunga timu hiyo ya Mauritius, itakutana na mshindi kati ya Mbabane Swallows ya Swaziland na APR ya Rwanda

CAF pia limeipangia Azam FC kusubiri mshindi kati ya Bidviets Witts ya Afrika Kusini dhidi ya bingwa wa Kombe la FA nchini Shelisheli.
Azam FC


Azam FC ndiyo wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Kombe la Shirikisho baada ya kushika nafasi ya pili msimu uliopita nyuma ya mabingwa Yanga.

Bingwa huyo wa FA wa Shelisheli anatarajia kupatikana wikiendi hii.

Iwapo Azam itashinda mechi yake hiyo ya kwanza, itakutana na vigogo Club Esperance de Tunis ya Tunisia
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment