KATIBU MKUU WA YANGA 'AJITUMBUA JIPU'



Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga Dr. Jonas Benedict Tiboroha ametangaza kujiuzulu wadhifa wake ndani ya klabu hiyo ya Jangwani kutokana na fukuto kubwa lililopo kwenye uongozi wa juu wa klabu hiyo.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyoandikwa kwenye ukurasa wa facebook wa ‘Naipenda Yanga’ ambapo kwa mujibu wa ukurasa huo, Dr. Tiboroha ametoa sababu kadhaa za kujiuzulu wadhifa wake ndani ya Yanga.

“Mimi ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kitivo cha Elimu ya Viungo (PE), na kwa kuondoka Yanga SC maana yake napata wasaa mzuri wa kumtumikia mwajiri wangu, UDSM,” amesema.

Pamoja na Tiboroha kutozama ndani sana juu ya kujiuzulu kwake, lakini inaelezwa alikuwa hana maelewano na Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya klabu ya Yanga, Isaac Chanji ambaye kwa sasa ndiye mtu anayesikilizwa na kuaminiwa zaidi na Yusufu Manji.

Tayari Jonas Tiboroha amewasilisha barua ya kujiuzulu kwa Mwenyekiti Yusuf Manji.

NB; KWA UNDANI ZAIDI SIKILIZA KIPINDI CHA MICHEZO CHA KUTOKA VIWANJANI CHA REDIO TUMAINI 96.5 FM
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment