KATIBU WA ZAMANI SIMBA SC AFARIKI DUNIA



Aliyekuwa katibu mkuu wa klabu ya soka ya Simba, Suleiman Said Suleiman maarufu kama Yelstin amefariki dunia.

Taarifa zinaeleza kuwa Yelstin ambaye hadi anakumbwa na mauti alikuwa ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), alikuwa akifanya mazoezi ya kuogelea na kisha kujihisi vibaya na kukimbizwa hoispitali.

Inaelezwa kuwa baada ya tukio hilo Suleiman alikimbizwa hospitali ya Agakhan kwa matibabu,na baadae ikaelezwa kuwa amekwishafariki dunia.
Marehemu aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa klabu hiyo katika miaka ya 1998-2000.

Wakati huohuo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetuma salamu za rambirambi kwa klabu ya Simba SC, kufuatia kifo cha Suleiman.

Katika salamu hizo TFF imesikitishwa na kifo cha kiongozi huyo, ambaye alingoza klabu ya Simba SC na kupelekea kupewa jina la utani la ‘Yelstin” kutokana na ufanisi wake katika kazi na misimamo akifananishwa na aliyekua Rais wa kwanza Urusi wakati huo Boris Yeltsin.

TFF kwa niaba ya familia ya mpira wa miguu nchini inawapa pole familia ya Seleman Said ‘Yelstin’ ndugu jamaa, marafiki, uongozi na wanachama wa klabu ya Simba kufuatia kifo hicho, na kusema wako pamoja katika kipindi hiki cha maombelezo.

Mazishi ya marehemu Selaman Said ‘Yelstin’ yalipangwa kufanyika leo saa 10 kamili jioni katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment