Lionel Messi ameshinda tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia kwa mara ya tano.
Messi amenyakua Ballon d’Or ya FIFA akiwabwaga wapinzani wake, Mbrazil Neymar anayecheza naye Barca na Cristiano Ronaldo wa Real Madrid katika hafla inayoendelea usiku huu mjini Zurich, Uswisi.
Lionel Messi amepata asilimia 41.33 ya kura zote akifuatiwa na Cristiano Ronaldo wa Ureno aliyepata asilimia 27.76, wakati Neymar anayeingia fainali kwa mara ya kwanza, amepata asilimia 7.86.
Mafanikio hayo yanakuja baada ya Messi kucheza mechi 53 mwaka jana akiwa na Barcelona, kufunga mabao 48 na kusababisha mabao 23, ingawa Cristiano Ronaldo alifanya vizuri zaidi, akifunga mabao 54 katika mechi 52 za Real Madrid.
WASHINDI KWA UJUMLA
Ballon d'or: Lionel Messi
Mchezaji Bora wa Kike wa Mwaka; Carli Lloyd
Tuzo ya Puskas: Wendell Lira
Kocha Bora wa Kiume wa Mwaka; Luis Enrique
Kocha Bora wa Kike wa Mwaka; Jill Ellis
Messi amenyakua Ballon d’Or ya FIFA akiwabwaga wapinzani wake, Mbrazil Neymar anayecheza naye Barca na Cristiano Ronaldo wa Real Madrid katika hafla inayoendelea usiku huu mjini Zurich, Uswisi.
Lionel Messi amepata asilimia 41.33 ya kura zote akifuatiwa na Cristiano Ronaldo wa Ureno aliyepata asilimia 27.76, wakati Neymar anayeingia fainali kwa mara ya kwanza, amepata asilimia 7.86.
Mafanikio hayo yanakuja baada ya Messi kucheza mechi 53 mwaka jana akiwa na Barcelona, kufunga mabao 48 na kusababisha mabao 23, ingawa Cristiano Ronaldo alifanya vizuri zaidi, akifunga mabao 54 katika mechi 52 za Real Madrid.
WASHINDI KWA UJUMLA
Ballon d'or: Lionel Messi
Mchezaji Bora wa Kike wa Mwaka; Carli Lloyd
Tuzo ya Puskas: Wendell Lira
Kocha Bora wa Kiume wa Mwaka; Luis Enrique
Kocha Bora wa Kike wa Mwaka; Jill Ellis

0 comments:
Post a Comment