MTOTO APEWA JINA LA ARSENAL BILA MAMA YAKE KUJUA



Imegundulika kuwa shabiki mmoja wa Arsenal alifanikiwa kumshawishi mkewe wampe mtoto wao jina la Arsenal bila mwanamke huyo kujua.

Ikumbukwe kuwa Arsenal ni jina la timu ya soka inayoshiriki Ligi Kuu soka nchini Uingereza na kwa sasa inaongoza katika msimamo.

Ilikuwa ni baada ya miaka miwili ambapo mwanamke huyo Clare Smith alijulishwa ujanja ambao mumewe alikuwa ametumia.

Bi Smith, kutoka eneo la Blacktown jimbo la New South Wales nchini Australia, alifichua hayo kwenye barua aliyoandikia jarida moja ambapo anasema mwenyewe hakugundua hilo hadi mumewe alipomwambia.

Amesema waliamua kumuita binti yao jina la Lanesra, kwa sababu lilikuwa jina la kipekee na la kupendeza lakini kumbe mumewe alitambua fika kwamba jina hilo likisomwa kutokea kulia kwenda kushoto lazima litamkwe Arsenal.

Habari kuhusu kisa hicho zimeenezwa sana mtandaoni, wengi wakijaribu kuandika majina ya klabu za Ligi ya Uingereza kutoka nyuma mfano Lanesra (Arsenal) na Retseciel (Leicester)

Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment