NADAL NAE ACHAKAZWA AUSTRALIAN OPEN



Rafael Nadal ameondolewa kwenye raundi ya kwanza katika mashindano ya tenisi ya Australian Open baada ya kufungwa kwa seti tano na Fernando Verdasco.

Hii ni mara ya kwanza kwa Nadal kuondolewa kwenye shindano katika raundi ya kwanza.

Wachezaji hao wawili kutoka Uhispania, wanaotumia mikono ya kushoto, walikabiliana katika uwanja wa Rod Laver Arena kwa zaidi ya saa nne na dakika 40.

Verdasco alishinda 7-6 (8-6) 4-6 3-6 7-6 (4-7) 6-2.

Mwanatenisi huyo aliyeorodheshwa nambari 45 duniani sasa atakutana na Dudi Sela kutoka Israel raundi ya pili.

“Nilicheza vyema sana raundi ya tano. Sijui nilifanikiwa vipi. Nilifunga macho yangu na kila kitu kikawa sawa,” amesema Verdasco, 32.

Verdasco alishindwa na Nadal nusufainali za 2009.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment