SIMBA SC 'MSITUNI' TENA LEO



Timu ya soka ya Simba usiku wa leo inashuka kwenye dimba la Amaan kucheza mchezo wake wa pili wa kundi A dhidi ya URA ya Uganda.

Mchezo huo utaanza saa 2:15 usiku ambapo Simba hadi sasa ina pointi moja baada ya sare ya 2-2 na Jamhuri ya Pemba katika mchezo wa kwanza huku URA ikiwa na pointi tatu baada ya juzi kuifunga JKU mabao 3-1.

Hali hiyo inailazimisha Simba ishinde mchezo wa leo ili iweze kusonga mbele, vinginevyo safari yake itaishia hapo.

Mchezo huo utatanguliwa na mechi ya mapema ya saa 10 jioni kati ya Jamhuri na JKU.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment