Baada ya safari yake kupigwa danadana kadhaa, hatimaye timu ya Yanga imepaa jioni hii kwenda Mauritius kwa ajili ya kucheza mechi yake ya kwanza ya mashindano ya Klabu bingwa Afrika dhidi ya Cecle de Joachim.
Yanga ambayo ilitua kwenye uwanja wa ndege wa JK Nyerere majira ya saa 9 usiku wa kuamkia leo, walijikuta wakikaa uwanjani hapo kwa zaidi ya saa 12 wakisubiri matengenezo ya ndege ya moja kwa moja waliyoikodi.
Mechi hiyo itapigwa kesho Jumamosi saa 9 alasiri kwa saa za Mauritius.
Yanga ilikuwa ipae tangu Jumatano iliyopita lakini safari iliahirishwa kwa lengo la kuepuka kuchosha wachezaji kwa ndege za kuunganisha.
Yanga ambayo ilitua kwenye uwanja wa ndege wa JK Nyerere majira ya saa 9 usiku wa kuamkia leo, walijikuta wakikaa uwanjani hapo kwa zaidi ya saa 12 wakisubiri matengenezo ya ndege ya moja kwa moja waliyoikodi.
Mechi hiyo itapigwa kesho Jumamosi saa 9 alasiri kwa saa za Mauritius.
Yanga ilikuwa ipae tangu Jumatano iliyopita lakini safari iliahirishwa kwa lengo la kuepuka kuchosha wachezaji kwa ndege za kuunganisha.

0 comments:
Post a Comment