MESSI AKUTWA NA TATIZO LA FIGO



Mshambuliaji wa klabu ya Barcelona Lionel Messi alikosa mazoezi siku ya Jumatatu ili kupimwa figo yake.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina alikosa kucheza mechi ya nusu fainali ya klabu bingwa duniani baada ya kupatikana na tatizo la figo,baada ya kuwa na maumivu ya tumbo yanayosababishwa na mawe ndani ya figo.

Hatahivyo alifanikiwa kushiriki katika fainali ya michuano hiyo siku tatu baadaye na ameichezea timu yake katika mechi zake zote za ligi.

Taarifa ya klabu ya Barcelona imesema kuwa Messi mwenye umri wa miaka 28 atarudi katika hali yake ya kawaida siku ya Jumatano.

Messi amefunga mabao 12 katika mechi 17 za ligi ya La Liga msimu huu na kuisaidia Barcelona kupanda pointi tatu juu ya jedwali la ligi hiyo.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment