SAFARI YA YANGA KWENDA MAURITIUS YAIVA


Na Arone Mpanduka
 
Kikosi cha wachezaji 21 wa timu ya soka ya Yanga kesho kitapaa kwenda nchini Mauritius kwa ajili ya mchezo wake wa kwanza wa Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Cercle de Joachim.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya Klabu hiyo yaliyoko mtaa wa Twiga na Jangwani jijini Dar es salaam, Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo Jerry Murro amesema Yanga itasafiri na watu saba wa benchi la ufundi na baadhi ya viongozi huku mkuu wa msafara akitarajiwa kuwa Ayoub Nyenzi kutoka Shirikisho la soka nchini TFF.

Amesema kwa mujibu wa taarifa walizopata kutoka Mauritius ni kwamba mchezo wao utachezwa Februari 13 mwaka huu.

Wakati hayo yakiendelea, Shirikisho la soka nchini TFF limezitakia kila lakheri timu zinazowakilisha nchi katika mashindano ya kimataifa ngazi ya vilabu.

Katibu mkuu wa TFF, Mwesigwa Celestine amesema jambo kubwa ambalo timu zinapaswa kufanya ni kuwa na nidhamu ili zifanikiwe katika michuano hiyo.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment