RAIS MPYA WA FIFA AKARIBISHWA KWA KIPUTE



Rais mpya wa Fifa, Gianni Infantino ametoa kali ya mwaka siku alipoingia ofisini baada ya kuamua apokelewe kwa kucheza mechi.

Wakati wengine wakitarajia aingie na kuanza kazi ofisini, yeye aliwaalika nyota wa zamani wa soka, halafu ikachezwa mechi.

Mechi ya kumpokea ilikuwa ni kati ya maofisa wa FIFA dhidi ya nyota hao, mechi iliyopigwa mwenye moja ya viwanja vilivyo katika ofisi za Fifa. 

Infantino mwenye miaka 45, aliwaalika nyota waliotamba zamani kama Deco, Luis Figo, Michel Salgado, Fabio Cannavaro, Paolo Maldini, Clarence Seedorf na wengine kwa ajili ya mechi hiyo ya burudani.

Infantino ameshinda urais wa Fifa kwa kupata kura 112 akichukua nafasi ya Sepp Blatter baada ya kumshinda rais wa Shirikisho la Soka la Bahrain, Sheik Salman bin Ebrahim Al Khalifa.

CHEKI JINSI ALIVYOKUWA AKISAKATA SOKA





Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment