AZAM YATOA NENO KUHUSU KAVUMBAGU






















Klabu ya soka ya Azam FC imekanusha taarifa ya kupokea maombi kutoka katika klabu mbalimbali za ndani na nje ya nchi ya kumuwania mchezaji wao Didier Kavumbagu katika dirisha dogo la usajili linalotarajiwa kufunguliwa hivi karibuni.

Akizungumza na waandishi wa habari mchana wa leo Afisa Habari wa Azam FC Jaffary Iddi amesema wao kama klabu bado hawajapata taarifa yoyote kuhusu mchezaji huyo hivyo bado ni mali yao.

“Tumekuwa tukisikia taarifa za mchezaji huyo zikizungumzwa sana, lakini sisi tunasema hazina ukweli wowote na Kavumbagu ni mali yetu,” alisema Jaffary.

Kwa kipindi kirefu Kavumbagu amekuwa akikalia benchi bila sababu ya msingi jambo ambalo hivi karibuni lilimfanya alalamike kwa vyombo vyahabari akidai hatendewi haki na kocha Muingereza Stewart John Hall.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment