BABU KIBADENI NA 'WAJUKUU' ZAKE WACHEMSHA ETHIOPIA



Timu ya taifa ya Tanzania Bara Kilimanjaro Stars leo imeshindwa kusonga mbele katika michuano ya Chalenji baada ya kutolewa nishai na timu ya Ethiopia kwa changamoto ya mikwaju ya penati 4-3 katika mchezo wa robo fainali uliopigwa mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.

Katika mchezo huo Kili Stars ilikuwa ya kwanza kupata bao lililofungwa na John Bocco katika dakika ya 24 ya mchezo.

Bao hilo lilipeta hadi dakika ya 57 ambapo Ethiopia walisawazisha kwa mkwaju penati uliofungwa na Panom na kufanya sare ya bao 1-1.

Sare hiyo ilidumu hadi dakika ya 90 zinamalizika na kwamujibu wa kanuni za mashindano hayo, katika hatua ya robo fainali lazima penati tano tano zipigwe ili kumpata mshindi, ndipo mwamuzi akaamuru penati hizo zipigwe.

Katika mikwaju hiyo ya penati tano tano, wachezaji wa Kili Stars Jonas Mkude na Shomari kapombe walishindwa kukwamisha wavuni penati zao na kuwafanya Wahabeshi hao watinge nusu fainali kwa penati 4-3.

Sasa Ethiopia itavaana na Uganda katika mchezo wa nusu fainali baada ya Uganda mchana wa leo kuichakaza Malawi mabao 2-0.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment