IVO SASA RUKSA KULA ICE CREAM ZA AZAM

Na Arone Mpanduka


Uongozi wa Azam FC umempa mkataba wa muda mfupi golikipa wa zamani wa timu za Tanzania Prisons, Yanga na  Simba  Ivo Mapunda baada ya kuridhishwa na uwezo wake.

Ivo alikuwa akifanya mazoezi ya kujiweka fiti na kikosi cha Azam baada ya kutemwa na klabu ya Simba kabla ya kuanza kwa msimu huu.

Akizungumza na MPANDUKA BLOG, msemaji wa Azam FC Jaffar Iddi amethibitisha taarifa hiyo ya kusajiliwa kwa Ivo Mapunda kujiunga na Azam kwa mkataba wa muda mfupi.

“Mkataba huu utampa uhuru wa kutoka na kwenda nje ya nchi endapo atahitajika na timu zingine kwa sababu alikwisha tutaarifu kuhusiana na uwezekano huo,”alisema Jaffar

Mapunda amekuwa akifanya mazoezi na klabu ya Azam kwa miezi mitatu sasa tangu alivyoachwa na klabu ya Simba kwa madai kwamba alikuwa akikwepa kusaini mkataba mpya aliokuwa akipewa na uongozi wa timu hiyo kitu ambacho Mapunda alisema si kweli.

Ivo Mapunda amewahi kuvitumikia vilabu kadhaa vya nje ya nchi ikiwemo St George ya Ethiopia pamoja na klabu ya Gor Mahia ya Kenya kabla ya kurejea nchini na kujiunga na ‘Wekundu wa Msimbazi’, Simba.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment