KAMATI YA TAIFA STARS YAVUNJWA

Baadhi ya wanakamati ya Taifa Stars, Michael Wambura(wa kwanza kushoto), Faroukh(katikati) na Teddy Mapunda (kulia)


Na Nicolaus Kilowoko

Siku chache baada ya timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kupoteza mchezo wake wa kusaka tiketi ya kushiriki fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Algeria, hatimaye hii leo Kamati ya kuisaidia timu hiyo yavunjwa rasmi.

Akizungumza na waandishi wa habari mchana wa leo(Nov 26,2015), Mwenyekiti wa kamati hiyo Faroukh Baghoza alisema muda wa kuendelea na kamati hiyo umekwisha kwa sababu kamati iliundwa kwa lengo la kuhakikisha timu inafanya vizuri dhidi ya Algeria na kwenda kwenye hatua ya makundi ya kusaka nafasi ya kushiriki kombe la dunia, kitu ambacho hakikuwezekana baada ya Stars kufungwa mabao 7-0.

Kwa  upande wa Makumu Mwenyekiti wa kamati hiyo Michael Wambura alisema anawashukuru Watanzania kwa umoja waliouonyesha kwa kuiunga mkono Taifa Stars katika  na kuwaomba kuendelea na moyo huo katika mechi zingine.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik alisema pamoja na kupoteza mchezo huo kwa magoli 7-0 dhidi ya Algeria lakini kiwango walichokionyesha Stars kilionyesha wazi kuwa kamati hiyo ili saidia vya kutosha timu hiyo
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment