NANI ATASONGA MBELE NA NANI YUKO HATARINI KLABU BINGWA ULAYA?



Baada ya mechi za jana na juzi za Champions League kinachofuata ni kuangalia nani ana nafasi ya kusonga mbele na nani yuko hatarini.

KUNDI A
Real Madrid inasonga mbele kama washindi wa kundi huku PSG ikisonga pia baada ya kumaliza ikiwa nafasi ya pili.

KUNDI B
Hadi sasa bado hakuna timu ‘inayosomeka’.Wolfsburg, Manchester United na PSV Eindhoven bado zinapambana zikiwania hizo nafasi mbili za juu za kutinga 16 bora.

KUNDI C
Timu za Atletico Madrid na Benfica zimejihakikishia kutinga 16 bora isipikuwa mechi zao za mwisho zitaamua nani anashika nafasi ya kwanza na nani anashika ya pili.

KUNDI D
Juventus na Manchester City nazo zote zimetinga 16 bora isipokuwa mechi zao za mwisho zitaamua nani anashika namba moja na nani ya pili.

KUNDI E
Barcelona katika kundi hili haina mpinzani, imesonga mbele moja kwa moja baada ya kuongoza kwenye kundi kwa pointi nyingi huku ikiwaacha Roma, Bayer Leverkusen na BATE Borislov zikigombania nafasi ya pili.

KUNDI F
Katika kundi hili Bayern Munich wamesonga mbele lakini nafasi ya pili bado inawaniwa na Arsenal na Olympiakos.

KUNDI G
Hapa timu mbili zina uhakika wa kusonga mbele kati ya Chelsea, Porto na Dynamo Kiev.

KUNDI H
Zenit St Petersburg imesonga mbele kama mshindi wa kundi na moja kati ya Gent ama Valencia itasonga mbele.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment