NYOTA WATATU ARSENAL WAPONA

Aaron Ramsey















Klabu ya Arsenal sasa imepata habari njema za kurejea dimbani kwa wachezaji wake watatu waliokuwa majeruhi.

Arsenal ilishindwa kupata matokeo mazuri katika michezo miwili mfululizo dhidi ya Bayern Munich na Tottenham Hotspur.

Kuelekea michezo ya kimataifa ya kalenda ya FIFA, Arsenal wamepata habari nzuri kutoka kwa wodi yao ya majeruhi baada ya taarifa za kupona kwa winga Oxlade Chamberlain, Aaron Ramsey na mlinzi Hector Bellerin ambao wanatarajiwa kurudi uwanjani baada ya wiki hiyo ya kimataifa.

Wachezaji hao mbali na Theo Walcott ambaye bado hayuko sawa, wanatarajiwa kupangwa katika mchezo wa ligi kuu nchini humo dhidi ya Westbromwich Albion wiki mbili zijazo.

Taarifa hizo ni nzuri kwa klabu ya Arsenal ambayo wiki mbili zijazo itapigana kugombania nafasi ya kufuzu hatua ya 16 ya michuano ya klabu bingwa barani Ulaya, mara baada ya kuwa imeshinda mchezo mmoja tu kati ya minne iliyocheza.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment