VIEIRA 'AULA' MAREKANI
















Klabu ya New York City inayoshiriki Ligi Kuu ya soka nchini Marekani maarufu kama ‘MLS’ imemteua mchezaji wa zamani wa klabu ya Arsenal na timu ya Ufaransa Patrick Vieira kuwa kocha mpya wa timu hiyo kuchukua nafasi ya kocha Jason Kreis.

Kabla ya kujiunga na timu ya New York City ,Vieira amekuwa kocha wa timu ya vijana na ile ya wachezaji wa akiba ya Manchester City nafasi ambayo amedumu nayo kwa muda wa miaka 5.

Klabu ya New York City haifanyi vizuri katika Ligi ya Marekani pamoja na usajili mubwa wa nyota wa soka duniani kama Frank Lampard mchezaji wa zamani wa vilabu vya West Ham United,Chelsea na Manchester City pamoja na Andrea Pirlo nyota wa zamani wa klabu za AC Milan na Juventus lakini bado timu hiyo imeshindwa kufuzu hatua ya mtoano ya Ligi ya Marekani.

Akizungumzia juu ya uteuzi wa Patrick Vieira kama kocha mpya wa klabu ya New York ,Rais wa klabu ya New York City Tom Glick anasema kuwa “uteuzi wa Vieira umezingatia vitu vingi vikiwepo nidhamu yake na mtazamo chanya aliokuwa nao wa kuifanya klabu ya New York City kuwa ya ushindani katika Ligi ya Marekani hapo baadae.”
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment