RONALDO 'ACHUMPA' KWENYE FILAMU





































Mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid ya Hispania, Cristiano Ronaldo usiku wa jana amefanya uzinduzi wa filamu yake iitwayo Ronaldo.

Uzinduzi huo umefanyika jijini London, England na kuhudhuriwa na wageni kadhaa huku kocha wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson akionekana kuwa mgeni aliyevutia zaidi.

Ronaldo alimkaribisha Ferguson kwa bashasha ikiwa ni pamoja na kumkumbatia.

Naye kocha Jose Mourinho aliyewahi kuwa bosi wa Ronaldo pale Real Madrid pia alijitokeza.

Wengine waliohudhuria katika uzinduzi huo ni Radamel Falcao, Carlo Ancelotti, Jorge Mendez, Garry Nevile pamoja na mtangazaji wa michezo wa kituo cha British Sports TV (Bt Sports) Hayley Mcqueen

Ronaldo aliongozana na mama yake mzazi, maria Dolores pamoja na mtoto wake, Ronaldo Jr.

Filamu hiyo iliyotengenezwa kwa zaidi ya miezi 14, imeongozwa na muongozaji muingereza Anthony Wonke ambayo maudhui yake makuu ni kuonyesha maisha ya nyota huyo tangu alipokuwa mtoto hadi sasa.
Jose Mourinho naye hakuwa nyuma
 
















Sir Ferguson naye alikuwepo kumsapoti kijana wake

Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment