TAIFA STARS YATOLEWA NISHAI NA VIJANA WA 'SAUZI'




































Taifa Stars imepoteza mechi yake ya kirafiki ya mazoezi dhidi ya timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 23 kwa kufungwa mabao 2-0.

Mechi hiyo imechezwa kwenye Uwanja wa Eldorado nje kidogo ya jiji la Johanesburg na muda mwingi vijana hao wanaofundishwa na Shau Bartlet aliyewahi kuchezea Charlton Athletic ya England na Bafana Bafana walitawala zaidi kipindi cha kwanza kwa kiasi kikubwa.

Baada ya mechi hiyo, Kocha Charles Boniface Mkwasa alisema wachezaji wake walicheza kwa tahadhari kubwa kwa hofu ya kuumia.

"Lakini kikubwa lilikuwa ni suala la mazoezi na kuangalia makosa ni nini na kipi cha kurekebisha," alisema Mkwasa.

Baada ya mechi hiyo, Stars imemaliza rasmi kambi yake ya hapa Afrika Kusini na kesho inaanza safari kurejea nyumbani.

Kikosi cha Kikosi kilichoanza leo:

1.   Aishi Manula
2.   Shomari Kapombe
3.   Haji Mwinyi
4.   Nadir Haroub
5.   Kelvin Yondani
6.   Jonas Mkude/Himid Mao
7.   Simon Msuva
8.   Salum Abubabary/Frank Domayo
9.   John Bocco/Elius Maguri
10.Mrisho Ngassa/Malimi Busungu
11. Farid Mussa/Salum Telela

CHANZO CHA HABARI; SALEH JEMBE BLOG
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment