CHELSEA KUMVUTA PEP GUARDIOLA



Bosi wa klabu ya soka ya Chelsea Roman Abramovich ana matumaini makubwa ya kumleta Pep Guardiola Stamford Bridge baada ya kuondoka kwa aliyekuwa kocha mkuu wa klabu hiyo Jose Mourinho,  kwa mujibu wa gazeti la Daily Mail.

Kocha huyo anayeinoa miamba ya soka nchini Ujerumani klabu ya Buyern Munich mkataba wake unaisha mwakani  na anaweza akatangazwa kuwa kocha wa Chelsea klabla ya mkataba wake haujaisha.

Kuna taarifa kuwa klabu ya Mancherster City inamyemelea  kocha huyo kuchukua mikoba ya Manuel Pellegrini lakini  Abramovich  aliyemtimua Jose Mourinho  Alhamis iliyopita anahitaji kumchukua kocha ndani ya klabu yake.

Bilionea huyo wa Urusi anajipanga kutumia fedha nyingi kwa ajili ya kuhakikisha kocha huyo mwenye miaka 44 anatua darajani.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment