KOMBE LA MAPINDUZI KUTIMUA VUMBI JANUARI 2 MWAKANI



Katibu Mkuu wa Chama cha Soka visiwani Zanzibar Kassim Haji Salum amesema timu za Gor Mahia ya Kenya , KCCA ya Uganda , Yanga, Simba, Azam FC na Mtibwa Sugar kutoka Tanzania Bara na Mafunzo na JKU kutoka visiwani Zanzibar ndio zitakazoshiriki mashindano ya Kombe la Mapinduzi.
Mashindano hayo yanatarajiwa kuanza rasmi Januari 2 mwakani visiwani humo.

Amesema michuano ya Mapinduzi Cup itazisaidia timu za Yanga, Azam FC, JKU na Mafunzo kujiandaa na Mashindano ya CAF ya vilabu Barani Afrika.

Yanga watacheza michuano ya Klabu Bingwa Afrika kwa mchezo wa mtoano na timu ya Cercle de Joachim ya Mauritius wakati Azam FC watacheza na mshindi kati ya klabu ya Seychelles na Bidvest Wits ya Afrika Kusini katika Kombe la Shirikisho.

Mafunzo ya Zanzibar, wao watacheza na klabu ya AS Vita ya Congo DR kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika na timu ya JKU itashiriki Kombe la Shirikisho pamoja na Gaborone United ya Botswana.


Hadi sasa Simba ndiyo mtetezi wa kombe hilo baada ya kushinda Januari mwaka huu kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Mtibwa Sugar.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment