YANGA YAFANYA HESABU ZA KUTOA NA KUJUMLISHA





Na Arone Mpanduka

Timu ya soka ya Yanga imeamua kuachana na mchezaji wake Mbrazil Andrew Countinho ili iweze kuongeza kifaa kingine kutoka nchini Niger Issouf Bubakar Garba, imefahamika.

Taarifa ambazo MPANDUKA BLOG imezinasa kutoka kwa mtu wa karibu wa timu hiyo, Countinho ameonekana kutowaridhisha viongozi wa Yanga hasa kufuatia kushuka kwa kiwango chake.

Kufuatia hali hiyo, Mbrazil huo ‘anakuwa mbuzi wa kafara’na kwa sababu pengo la mchezaji mmoja litakuwepo, Yanga watalazimika kulitumia vema dirisha la sasa la usajili kwa kumleta Mniger huyo.

Hata hivyo MPANDUKA BLOG iliamua kwenda mbali zaidi na kuwatafuta wahusika ambapo Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro alionekana kujibu kwa kusitasita, jambo ambalo limeonyesha kuwa na ukweli isipokuwa klabu haijajiandaa kutoa taarufa rasmi kwa sasa.

“Huenda taarifa hizo zikawa hazina ukweli ama kwa upande mwingine pia zikawa kweli lakini niwahakikishie wana Yanga kwamba siku ya Ijumaa tutafanya mkutano na waandishi wa habari na kuwaeleza kila kitu”
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment