KOLO: UWANJA WA EMIRATES UNAINYIMA UBINGWA ARSENAL




Beki wa zamani wa Arsenal, Kolo Toure amesema Uwanja wa Emirates ndio chanzo kikubwa cha klabu hiyo kushindwa kunyakuwa taji la Ligi Kuu katika kipindi cha miaka 10 iliyopita. 

Arsenal walikuwa wakitumia Uwanja wa Highbury kabla ya kuamua kujenga uwanja mpya wenye uwezo wa kubeba mashabiki 60,000 ambao walihamia mwaka 2006. 

Taji la mwisho la ligi kuchukuliwa na Arsenal ilikuwa msimu wa 2003-2004 wakati klabu hiyo ilipomaliza msimu bila kufungwa na wamenyakuwa mataji manne pekee toka wakati huo. 

Lakini Toure amempongeza meneja wa timu hiyo Wenger kwa juhudi zake toka wakati huo baada ya klabu kulazimika kupunguza matumizi kwa miaka kadhaa ili kuweka mahesabu yao sawasawa. 

Toure amesema ingawa hayuko katika klabu hiyo lakini kuna mambo mengi yalibadilika, wachezaji wengi waliondoka akiwemo Patrick Vieira hivyo iliwawia vigumu lakini sera hiyo ilianza wakati wameanza ujenzi wa uwanja mpya. 

Toure aliendelea kudai kuwa Arsenal ililazimika kuuza nyota wake akiwemo Robert Pires, Thiarry Henry na kulazimika kuanza kutegemea wachezaji chipukizi wasiokuwa na uzoefu wowote.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment