UBINGWA KWA LEICESTER CITY, 'MIJIHELA' KWA SHABIKI



Shabiki mmoja wa klabu ya Leicester City huenda akajishindia pauni 25,000 iwapo timu hiyo itashinda taji la Ligi kuu ya Uingereza baada ya kuweka pauni tano katika dau la paundi 5,000.

Ushindi wa Leicester wa mabao 3-1 dhidi ya Manchester City unawaacha wakiwa mbele kwa pointi tano katika msimamo wa Ligi huku Ligi hiyo ikiwa imefikia kwenye robo tatu ya mechi zake.

Carpenter Leigh Herbert, mwenye umri wa miaka 38 alijaribu bahati hiyo akiwa katika likizo na amekataa ombi la kumtaka achukue pauni 3,200 ili kujiondoa.

Iwapo Leicester ambao walikuwa chini ya msomamo wa ligi hiyo mwaka mmoja uliopita watashinda taji hilo la ligi,inaaminika kuwa hiyo itakuwa zawadi kubwa kuwahi kutolewa katika historia ya michezo.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment