SAMATTA AONJA KICHAPO CHA KWANZA ULAYA

Mshambuliaji wa Tanzania Mbwana Samatta ameambulia kichapo cha kwanza akiwa Ulaya na klabu yake ya Genk baada ya timu hiyo kuchapwa bao 2-1 na klabu ya Standard Liege kwenye mchezo wa ligi kuu ya Belgium uliochezwa usiku wa Jumamosi ya Machi 5.

Genk wakiwa ugenini ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 42 kipindi cha kwanza likifungwa na Nikolaos Karelis na kuipeleka Genk mapumziko ikiwa kifua mbele kwa bao 1-0.

Dakika tatu baada ya kipindi cha pili kuanza, Ivan Santini akaisawazishia Standard Liege kabla ya Jean-Luc Diarra Dompe kuifungia Standard bao la ushindi na kupeleka msiba kwa Genk.

Kama kawaida Samatta iliingia uwanjani dakika ya 81 kuchukua nafasi Karelis lakini bado haikutosha kubalili matokeo.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment