Genk wakiwa ugenini ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 42 kipindi cha kwanza likifungwa na Nikolaos Karelis na kuipeleka Genk mapumziko ikiwa kifua mbele kwa bao 1-0.
Dakika tatu baada ya kipindi cha pili kuanza, Ivan Santini akaisawazishia Standard Liege kabla ya Jean-Luc Diarra Dompe kuifungia Standard bao la ushindi na kupeleka msiba kwa Genk.
Kama kawaida Samatta iliingia uwanjani dakika ya 81 kuchukua nafasi Karelis lakini bado haikutosha kubalili matokeo.
0 comments:
Post a Comment