SIMBA SC YAZIDI KUPAA




Simba imeendeleza wimbi la ushindi Jumamosi ya leo kwa kuifunga Coastal Union mabao 2-0. 

Mabao ya Danny Lyanga na Hamis Kiiza yameipa Simba pointi tatu kwenye uwanja wa Mkwakwani na sasa imefikisha jumla ya pointi 57 baada ya kucheza michezo 24 ya ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Simba sasa inaongoza ligi kwa tofauti ya pointi saba dhidi ya wapinzani wake kwenye mbio za ubingwa Yanga na Azam zenye pointi 50 kila moja huku zikiwa zimecheza mechi 21 mechi tatu nyuma ya Simba.

Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment