YANGA YAITUPA APR, YASONGA MBELE





Yanga SC Jumamosi ya leo imesonga mbele kwenye michuano ya klabu bingwa Afrika licha ya kutoka sare ya 1-1 APR ya Rwanda kwenye mchezo wa marudiano uliopigwa kwenye dimba la Taifa jijini Dar es Salaam.

APR  ambao walipoteza mchezo wa kwanza kwa mabao 2-1 jijini Kigali, waliwashtua Yanga mapema katika dakika ya tatu baada ya winga Fiston Nkinzingabo  kuifungia timu yake bao zuri akimalizia krosi ya Rusheshangonga Michel.

Bao hilo halikudumu sana kwani dakika ya 28 ya mchezo, Donald Ngoma alisawazisha na kufanya sare hiyo idumu kwa kipindi chote cha dakika 90.
Yanga imesonga mbele kwa jumla ya mabao 3-2 baada ya mchezo wa awali kushinda ugenini 2-1.

Baada ya mchezo kumalizika Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga , Jerry  Murro alikiri kamba mchezo ulikuwa mgumu na kuongeza kwamba sasa wanageukia viporo vyao vya Ligi Kuu Tanzania Bara.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment