VIJEMBE VYA MANARA, MURO VYAFIKIA PABAYA



MKUU wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Klabu ya Simba, Haji Manara amelalamikia tabia ya Mkuu wa Habari wa Yanga Jerry Muro kuendelea kumpiga vijembe vinavyolenga kumdhalilisha kupitia vyombo vya habari.

Akizungumza hivi karibuni kupitia kituo cha Redio cha EFM, Manara alikilaumu kituo hicho kwa kumpa muda wa maongezi Jerry ambaye aliutumia kwa kutoa kauli za kumdhalilisha.

Manara alisema ameumizwa na kitendo cha Jerry kutamka hewani kwamba amekuwa akiwashwa washwa kwa kufuatilia mambo ya Yanga ambayo hayamuhusu.

“Anatumia muda mwingi sana kumzungumzia Haji na maisha yake na cha ajabu mmenisikitisha sana kumruhusu anidhalilishe, ataniambiaje mimi ninawashwa na nataka kukunwa? Hebu angalieni vitu vingine vya kurusha hewani.Ni vizuri ndugu yangu akazungumzia zaidi mpira badala ya mtu binafsi”

“Ninachojaribu kulia na Yanga siku zote si kuisemea bali ni kuzungumzia uhalisia wa kile kinachoendelea hasa wingi wa mechi zao za viporo.Duniani kote umeona wapi timu inacheza mechi tatu mfululizo za viporo?Hiyo ndiyo hoja yangu ya msingi, na siku zote nitabaki kuwa muungwana na wala sitomjibu,”alisema Manara.

Manara aliyasema hayo ikiwa ni siku moja baada ya Jerry kutoa kauli hizo hewani huku kisa kikiwa ni uwepo wa mechi nyingi za viporo za Ligi Kuu kwa Yanga ambayo inashiriki mashindano ya Klabu Bingwa Afrika.
Share on Google Plus

About MPANDUKA BLOG

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment